Rosie na Ruby Formosa walikuwa
wameungana kwenye sehemu yao ya tumbo na walitumia sehemu moja ya utumbo
waliyotumia kabla ya kufanyiwa upasuaji wa dharura wa kuwatenganisha mnamo
mwaka 2012.
Mama yao , Angela Formosa, amesema
watoto hao ambao kwa sasa wana umri wa miaka minne , kutoka eneo la la
Bexleyheath Kusini mashariki mwa mji wa London ,"wanafuraha sana " ya
kuanza shule.
Miaka mmine iliyopita akilini mwangu
sikufikiria kitu kama hiki kingelitokea ," alisema.
"Nilipokuwa mjamzito sikudhani
nitaiona siku ya ya kwanza shuleni kwa hivyo inanifurahisha sana kwa hiyo
nashukuru sana hospitari ya I Gosh [Great Ormond Street Hospital] kwa kweli.
Nilipokuwa mjamzito sikudhani
nitaiona siku ya ya kwanza shuleni kwa hivyo inanifurahisha sana kwa hiyo
nashukuru sana hospitari ya I Gosh [Great Ormond Street Hospital] kwa
kweli."
Bi Formosa alisema ilikuwa ni taarifa
ya ''kuvunja moyo'' kwake na kwa mumewe Daniel Formosa walipogundua kuwa watoto
wao wa kike walikuwa na hali ya nadra ya kimatibabu, ambayo hutokea mara moja
kati ya watoto 200,000 hai wanaozaliwa .
Watoto hawa wa kike walizaliwa katika
hospitali ya Uversity College of London kwa upasuaji mwaka 2012 wakati mama yao
Bi Formosa akiwa na ujauzito wa wiki 34.
Baada ya saa kadhaa baada ya kuzaliwa
walipelekwa katika hospitali ya Great Ormond Street Hospital kwa ajili ya
upasuaji wa dharura kutokana na kuziba kwa utumbo.
Bi Formosa, mwenye umri wa miaka 35,
anasema alihisi ni kama " miaka milioni "iliyopita kuwasubiri watoto
hao kutoka kwenye chumba cha upasuaji .
" Muda umekwenda, siwezi kuamini
jinsi muda ulivyokwenda haraka ," alisema.
" Wanafanana sana, wanaakili
sana na bidii , ambayonaifahamu walikua nayo ndani ya tumbo yangu kwa sababu
waliendelea kukua na kujitahidi kuishi
Profesa Paolo De Coppi, mtaalamu wa
upasuaji wa watoto katika hospitali ya Gosh, amesema : "Tunafurahi kwamba
Rosie na Ruby wanaanza shule Septemba mwaka huu.
Visa vya watoto kuzaliwa wakiwa
wamegandana hutokea mara kwa mara katika nchi tofauti huku madaktari na
wanasayansi wakifanya juhudi zote kuhakikisha wanaokoa maisha ya watoto hao
No comments:
Post a Comment