Na Anael James
Klabu ya
wagonga nyundo wa jiji la Mbeya wanatarajiwa kuongoza ligi endapo watashinda
mchezo wao wa leo utakaopigwa muda si mrefu jijini Mwanza na klabu ya MBAO FC
ya jijini Mwanza.
Mbeya CITY
wakiwa na pointi nne sawa na Simba SC,Azam FC,Ruvu Shooting na Prison leo
itakaa kileleni endapo itashinda au kutoka sare kutokana na timu zilizojuu
hazitacheza leo hadi hapo badae.
Kocha wa
Mbeya CITY,Kinnah Phiri amesema kuwa kikosi chake kipo vizuri na wanatarajia
kuongoza ligi.
Mbali na
hapo kocha wa Mbao FC,Ndairagaje Etiene, amesema kuwa timu yake ipo nafasi
mbaya sana katika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi hivyo kuna ulazima mkubwa
wa kushinda.
No comments:
Post a Comment