NYOTA wa zamani wa
kimataifa wa Brazil na klabu za Barcelona na AC Milan, Ronaldinho
amebainisha nia yake ya kutaka kutundika daruga zake baada ya kupita
miaka 18 akisakata kabumbu barani Ulaya na Amerika Kusini. Mkongwe huyo
mwenye umri wa miaka 36, ni mmoja kati ya wachezaji wachache kuwahi
kunyakuwa mataji ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na lile la Copa Libertadores
na pia amewahi kutwaa Kombe la Dunia akiwa na Brazil mwaka 2002. Lakini
kushindwa kwake kutulia katika klabu moja toka alipoondoka Atletico
Mineiro mwaka 2014 kunamfanya kufikiri kuwa wakati wake wa kustaafu
umefika. Akizungumza na wanahabri jijini New York, Ronaldinho amesema
kwasasa ameshakuwa mtu mzima na sio Ronaldinho yule aliyekuwa na miaka
26 waliyemzoea. Nyota huyo alindelea kudai kuwa anadhani wakati wake wa
kustaafu umefika na atafanya hivyo baada ya kucheza kwa kipindi cha
mwaka mmoja zaidi.
Make Money Online : http://ow.ly/KNICZ
Na Babu AllyMake Money Online : http://ow.ly/KNICZ
Vanessa Mdee amefunguka sababu inayomfanya awe na ziara za mara kwa mara kwenye vyombo vya habari vya nchi za nje ikiwemo Nigeria na nchi nyingine anazopendelea kwenda.
Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha East Afrika Television kuwa anafanya sana media tour kwenye nchi nyingine kwakuwa inamsaidia kupata mashabiki wengi zaidi.
“Unajua nafanya sana media tour, kwani wenzetu ni wazito sana kupokea kazi za wasanii wa nje ya kwao. Hivyo hizo media tour zinanisaidia kujenga fan base katika nchi zao,” amesema Vee Money.
Vee Money ni mmoja kati ya wasanii wachache wa Bongo Fleva waliofanikiwa kupata collabo na wasanii wa nje akiwa tayari ameshafanya kazi na wasanii kutoka nchi tofauti topfauti ikiwemo Nigeria, Togo, Malawi, Ufaransa na sehemu zingine.
No comments:
Post a Comment