Mamia ya wachuuzi waliokasirika wamefanya maandamano katika barabara za eneo la Eastleigh jijini Nairobi ili kupinga kuvunjwa kwa vibanda vyao.
Usiku kucha
maafisa wa polisi waliharibu vibanda vilivyojaa kandokando ya barabara ambapo
huweka bidhaa zao zote.
Operesheni
hiyo ya polisi inafuatia malalamishi kutoka kwa wamiliki wa maduka ambao
wanasema kuwa wamekuwa wakizuia watu kuingia katika maduka hayo.
Wamiliki wa
maduka pia nao wamefunga maduka yao ikiwa ni mgomo wao wa siku tatu wa kutaka
baraza la jiji la Nairobi kuwandoa wachuuzi hao.
Visa kama
hivi vimekuwa vikitokea mara kwa mara katika mji wa Nairobi huku serikali
ikitupiwa kidole cha lawama.
No comments:
Post a Comment