Na MustafaIsmail
WANAFUNZI 15
wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Usevya wilayani Mlele Mkoa wa Katavi
wameamriwa kurejea nyumbani kwa wiki mbili kwa kosa la kuwashambulia kwa
kuwacharaza viboko walimu wao wawili akiwemo Makamu Mkuu wa Shule, Makonda
Ng’oka ‘Membele’ (34) ambaye ameng’olewa meno matano kwa kipigo hicho.
Aidha,
wanafunzi hao wanaodaiwa kuwa vinara wa mkasa huo wametakiwa kulipa faini ya Sh
20,000 kila mmoja wao na wametakiwa kuzilipa mara watakaporejea shuleni.
Taarifa
kutoka shuleni hapo zinaeleza kuwa kikao cha Bodi ya Shule hiyo kilichokutana
mwishoni mwa wiki, kilitoa adhabu hizo kwa wanafunzi hao ikiwataka wasionekane
shuleni hapo kwa kipindi cha wiki mbili.
Ofisa Elimu
wa Mkoa wa Katavi, Ernest Hinju amethibitishwa kufukuzwa kwa wanafunzi hao
akisema kuwa Bodi ya shule hiyo iliketi Septemba 16, mwaka huu shuleni hapo na
kufikia maamuzi hayo huku akisisitiza kuwa maelezo zaidi atatoa baadaye.
Walimu hao
wawili wameendelea kusisitiza kuwa kuwa hawako tayari kuendelea kufundisha
katika shule hiyo huku wakisisitiza kuwa ni fedheha kwao kucharazwa viboko na
wanafunzi wao wenyewe, huku mwalimu Gabriel Kambona akiachwa na ngeu kichwani.
Mwalimu Kambona alidai kuwa
haridhiki na adhabu waliopewa wanafunzi hao.
Chanzo Habari leo
haridhiki na adhabu waliopewa wanafunzi hao.
Chanzo Habari leo
No comments:
Post a Comment