Na Anael James
KLABU ya Borussia Dortmund jana ilifanikiwa kuigaragaza
Legia Warsaw ya Poland kwa mabao 8-4 na kuweka historia ya kuwa mchezo
uliofungwa mabao mengi zaidi katika historia ya michuano ya Ligi ya Mabingwa
Ulaya.
Jumla ya mabao 12 yalifungwa katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja
wa Westfalen na kuipita rekodi ya ya mabao 8-3 ya Monaco dhidi ya Deportivo La
Coruna mwaka 2003.
Mpaka dakika ya 22 kipindi cha kwanza tayari yalikuwa
yameshafungwa jumla ya mabao saba, wakati Marco Reus akiifungia hat-trick
Dortmund.
Legia pia inakuwa klabu ya kwanza katika historia ya michuano hiyo
kufunga mabao manne halafu kuja kupoteza mchezo
No comments:
Post a Comment