DORTIMUND WAWEKA REKODI MPYAA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Wednesday, November 23

DORTIMUND WAWEKA REKODI MPYAA

Na Anael James

KLABU ya Borussia Dortmund jana ilifanikiwa kuigaragaza Legia Warsaw ya Poland kwa mabao 8-4 na kuweka historia ya kuwa mchezo uliofungwa mabao mengi zaidi katika historia ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. 


Jumla ya mabao 12 yalifungwa katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Westfalen na kuipita rekodi ya ya mabao 8-3 ya Monaco dhidi ya Deportivo La Coruna mwaka 2003.

Mpaka dakika ya 22 kipindi cha kwanza tayari yalikuwa yameshafungwa jumla ya mabao saba, wakati Marco Reus akiifungia hat-trick Dortmund. 

Legia pia inakuwa klabu ya kwanza katika historia ya michuano hiyo kufunga mabao manne halafu kuja kupoteza mchezo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here