Taarifa zinaripoti kuwa wafungwa zaidi ya 20 wametoroka katika magareza Ijumaa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Wafungwa hao wameripotiwa kutoka katika gereza la Bukavu Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Meya wa jiji la Bukavu Philemon Yogolelo aliliambia shirika la habari la Anadolu kuwa mfungwa mmoja alifariki katika tukio hilo.
Wafungwa wengine wane walijeruhiwa walipokuwa wakijaribu kutoroka.
No comments:
Post a Comment